WAZIRI BASHE AKIWASILISHA BAJETI WIZARA YA KILIMO 2022.
“Serikali ya Awamu ya Kwanza, ilitambua Tanzania kama nchi ya Wakulima na Wafanyakazi na kuwekeza katika kilimo hususani katika maeneo ya:- Vyuo vya Utafiti na Mafunzo, Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo, Mashirika ya Umma yanayosimamia Kilimo, Bodi za Mazao na Vyama vya Ushirika.” “Pia ilihamasisha kilimo na lishe kupitia programu na kampeni mbalimbali ikiwemo Ukulima wa Kisasa, Kilimo cha kufa na kupona, Chakula ni Uhai, Mtu ni Afya, Elimu ya Kujitegemea na Siasa ni Kilimo. Aidha, katika kipindi hicho, msisitizo uliwekwa katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara na kufikia kiwango cha kuongoza kimataifa kwa baadhi ya mazao ikiwemo korosho na mkonge” “Serikali ya Awamu ya Pili, ilifanya mageuzi ya uchumi yaliyokuwa kichocheo katika maendeleo ya kilimo ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa Sera ya Kilimo ya mwaka 1983. Aidha, Serikali ilipunguza vikwazo katika biashara ili kurahisisha upatikanaji wa bidhaa kwa ajili ya ustawi wa wananchi.” “Serikali ya Awamu ya Tatu, iliimarisha Taa...